Kurasa.

Makubaliano ya Waandishi na Affiliates

Haya ni makubaliano kati yako (mwandishi au mshirika) na Kurasa. Tafadhali yasome kwa makini kabla ya kujiunga.

1. Mgao wa mapato

  • Mwandishi hupata 60% ya kila malipo yanayotokana na hadithi zake; Kurasa hubaki na 40% kugharamia mfumo wa malipo, tovuti na uendeshaji.
  • Affiliate hupata kamisheni ya 15% kwa malipo ya kwanza ya kila mtu anayejiunga kupitia link yake, na 8% kwa malipo yanayorudia.
  • Asilimia hizi zinaweza kubadilika; utajulishwa kabla ya mabadiliko.

2. Ratiba ya malipo (kila wiki)

  • Kipindi cha mahesabu: Jumamosi 00:00 hadi Ijumaa 23:59.
  • Malipo hufanyika Jumatatu kwa mapato ya wiki iliyoisha.
  • Salio la kipindi kipya huanza kuonekana kila Jumamosi 00:00.
  • Kiasi kilicho chini ya kiwango cha chini cha malipo hubaki (hakipotei) na huongezwa kwenye wiki inayofuata.

3. Akaunti ya malipo

  • Unaweka namba ya akaunti yako ya malipo (M-Pesa, Tigo Pesa au Airtel Money) mara moja.
  • Baada ya kuiweka, huwezi kuibadilisha mwenyewe. Ukihitaji kubadilisha, wasiliana na Kurasa kwa info@kurasa.co.tz kabla ya Jumamosi 00:00.
  • Mabadiliko ya akaunti yanaruhusiwa mara moja tu kwa mwezi.
  • Ni wajibu wako kuhakikisha namba ni sahihi. Kurasa hawajibiki kwa malipo yaliyotumwa kwa namba uliyoitoa.

4. Wajibu wa mwandishi

  • Hadithi lazima ziwe kazi yako halisi — usiibe wala kunakili kazi ya mtu mwingine.
  • Hadithi zisiwe na maudhui haramu, ya chuki, au yanayokiuka sheria za Tanzania.
  • Kurasa inaweza kuondoa hadithi inayokiuka masharti bila taarifa.

5. Wajibu wa mshirika

  • Usidanganye mfumo — kubofya link yako mwenyewe au kutumia namba za uongo kunaweza kufuta kamisheni na akaunti yako.
  • Usisambaze link kwa njia za spam au udanganyifu.

6. Kodi na mengineyo

  • Wewe unawajibika kwa kodi zozote za mapato yako kwa mujibu wa sheria.
  • Kurasa inaweza kusitisha ushiriki wako kwa ukiukaji wa masharti haya.

Una swali kuhusu makubaliano haya? Wasiliana nasi kwa info@kurasa.co.tz.